4x4

MUHTASARI WA HOTUBA YA RAIS DK MAGUFULI KWENYE MAADHIMISHO YA MIAKA 55 YA UHURU, DESEMBA 9, 2016

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
Description: Description: Description: Description: Description: Coat of ArmsKURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU
Simu: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Tovuti : www.ikulu.go.tz              

Faksi: 255-22-2113425


OFISI YA RAIS,
      IKULU,
 1 BARABARA YA BARACK OBAMA,  
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi mkuu Dkt. John Pombe Magufuli leo Ijumaa ya tarehe 09 Desemba, 2016 amewaongoza viongozi mbalimbali na wananchi kwa ujumla katika maadhimisho ya miaka 55 ya Uhuru wa Tanzania Bara .

Maadhimisho hayo ya miaka 55 ya Uhuru wa Tanzania Bara yamefanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es salaam na kupambwa na gwaride maalum lililoandaliwa kwa pamoja na Majeshi ya Ulinzi na Usalama ikiwa ni pamoja na Jeshi la wananchi wa Tanzania JWTZ,Jeshi la Polisi,Jeshi la Magereza na Jeshi la Kujenga Taifa.

Akizungumza na halaiki ya watanzania waliohudhuria sherehe hizo Rais Dkt Magufuli amesema mwaka jana alilazimika kuzuia kufanyika kwa shamrashamra ya maadhimisho ya Uhuru wa Tanzania Bara kutimiza miaka 54 kwa kuwa alikuwa na mwezi mmoja tu tangu aingie madarakani na kuitaja sababu ya pili kuwa ni  bajeti kubwa ya shilingi bilioni nne iliyokuwa imetengwa kwa ajili ya maadhimiso hayo na kuona ni vyema ikaelekezwa katika upanuzi wa barabara ya Alli Hassani Mwinyi yenye urefu wa kilomita 4 ambayo inatumiwa na Watanzania wote badala ya fedha zile kutumiwa na wachache.

"Sherehe za miaka 55 nimeamua zifanyike kwasababu gharama zake ni ndogo sana,kwanza hakuna hata chakula baada ya sherehe hii,hakuna dhifa ya Taifa ,tukimaliza hapa tumemalizana ,lakini pili niliamua sherehe hii niifanye hapa Dar es Salaam kwa kuwa yatakuwa ni maadhimisho ya mwisho kufanyika jijini Dar es salaam na kwamba ni matumaini yake kuwa sherehe za mwaka kesho zitafanyika makao makuu ya nchia mbayo ni Dodoma"

Ameongeza kuwa sherehe za Uhuru ni tukio kubwa sana katika Taifa na hivyo serikali itaendelea kuipa umuhimu siku hiyo na kuiadhimisha.

Rais Dkt Magufuli pia amezitaja changamoto ambazo serikali ya awamu ya tano inazokumbana nazo kuwa ni pamoja na ufisadi na rushwa ndani ya baadhi ya watendaji na kuongeza kuwa mpaka sasa hivi wafanyakazi hewa wamefikia elfu kumi na tisa huku kaya masikini hewa zinazonufaika na mfuko wa TASAF zikiwa ni elfu 55 na wanafunzi hewa  mpaka sasa hivi wamefikia elfu sitini na tano

"Serikali ya awamu ya Tano itaendelea kuchukua hatua kali ikiwa ni pamoja na kuwatumbua hadharani wale waliozoea kutumbua hadharani mali za watanzania na tuataendelea kuchukua hatua kali katika masuala ya rushwa na ufisadi,kwasababu rushwa ni saratani"

Rais Dkt Magufuli amepongeza pia jitihada zilizofanywa na watangulizi wake katika maendeleo ya Tanzania na kuwashukuru kwa niaba ya watanzania huku akiwataka watanzania wote bila ya kujali dini,itikadi za kisiasa  na makabila yao kuendelea kudumisha amani na mshikamano ili Tanzania iweze kupiga hatua za kimaendeleo kwa haraka.

"Hivyo basi tuendelee kuilinda amani yetu na kuwafichua watu wenye nia ovu ya kuhatarisha amani yetu na sambamba na kulinda amani yetu hatuna budi kudumisha umoja na mshikamano wetu ambao ni nguvu na silaha yetu kubwa kama Taifa,lakini pia tuendelee kuulinda muungano wetu ambao ni silaha kubwa ya umoja wetu ili Tanzania tuendelee kwenda mbele"

Hii ni mara ya kwanza kwa Rais Dkt John Pombe Magufuli kuhudhuria na kuhutubia katika sherehe za Uhuru wa Tanzania Bara tangu aingie madarakani.


Emmanuel Buhohela
Kaimu Mwandishi wa habari Msaidizi wa Rais.
Dar es Salaam
09 Desemba, 2016





0 comments:

Post a Comment